Kwa mujibu wa Kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, Hujjatul-Islam wal-Muslimin Sayyid Sadruddin Qabanchi, Imamu wa Ijumaa wa Najaf Ashraf, katika kongamano la Muballeghina lililoandaliwa na Ofisi ya Imamu wa Ijumaa wa Najaf Ashraf kwenye Husseiniya Fatimiya, kwa ushiriki mpana wa walinganiaji wanaume na wanawake katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, alisisitiza kuwa: Sisi ni wa kimataifa kwa sababu Uislamu ni wa kimataifa. Tunahitaji kuhuisha zana zetu za tablighi. Mwanazuoni wa dini anapaswa kuwa na nguvu ya kuvutia iliyo kubwa kuliko nguvu ya kufukuza.
Aliongeza kuwa: Haijuzu kuwa na shaka juu ya taifa la Iraq, utambulisho wake na uaminifu wake. Uzoefu wetu nchini Iraq baada ya kuanguka kwa twaghuti ulikuwa uzoefu wenye mafanikio, ingawa uliambatana na changamoto kubwa. Haifai kutilia shaka uzoefu huu, hata kama kulikuwa na makosa, kama Qur’ani Tukufu inavyosema:
“Kwa hakika mema huondoa maovu.”
Katika kongamano hili, Hujjatul-Islam wal-Muslimin Sayyid Sadruddin Qabanchi alisisitiza umuhimu wa kuimarisha uaminifu na mtazamo chanya kwa taifa la Iraq licha ya taabu zote, na akasema: Uzoefu wa Iraq baada ya kuanguka kwa twaghuti ni uzoefu wenye mafanikio katikati ya changamoto na matatizo makubwa.
Pia alisisitiza umuhimu wa kuwa na mtazamo wa baadaye na upeo wa kimataifa, akisema: Uislamu wetu ni dini ya kimataifa. Leo tumeingia katika uzoefu mpya nchini Iraq, lakini malengo yetu yanavuka mipaka na yanaenea ulimwenguni kote, na muendelezo wake utaendelea hadi kudhihiri kwa Hadhrat Baqiyyatullah al-A‘dham (Mwenyezi Mungu aharakishe faraja yake tukufu), ambaye ataujaza ulimwengu uadilifu na usawa baada ya kujazwa dhulma na uonevu. Kwa hiyo, si sahihi kujifunga katika mipaka ya kijiografia au kikabila.
Mwisho, Imamu wa Ijumaa wa Najaf Ashraf alisikiliza hotuba na mitazamo ya baadhi ya walinganiaji wanaume na wanawake, na akashiriki nao katika mazungumzo huru na ya kirafiki.
Maoni yako